Usiku wa harusi yangu

Ads related

( USIKU WA HARUSI YANGU) Chombezotu.blogspot.com SEHEMU YA................... 01 " Nimekuelewa mama, sawa mama, nawezaje kukataa jambo jema kama hilo? Namaanisha nimekubali moja kwa moja." Ni sauti ya binti mmoja mrefu wa mnene kiasi, nikisema mnene kiasi namaanisha ana shepu la kihaya. Mnayajua mashepua ya kihaya nyie. Ndo huyu binti aliekua katupa mgongo akiongea na simu alikuwa na shepu hilo, mshepu namba nane, huku nywele zake nyeusi zikining'inia kwenye mabega yake, alikuwa kavaa gauni la kijani kibichi lililombana kiasi kwamba tuliweza kuiona shepu yake vyema. Miguu yake minene na mzuri yenye utege wa kulegeza nyonga iling'aa kwa rangi nzuri ya chocolate, ukimwangalia hivyo tu unakubali mwenyewe kwamba dada yule ni dada wa kishuaa dada wa kitajiri. " maisara bado unaongea na simu" alitokea binti mmoja aliejulikana kwa jina la Zawadi, akiwa kavaa miwani wa mikanda mieusi mipana na mviringo. Alimfanya Maisara ageuke na tuweze kuujua uso wake vyema ni jinsi gani alikuwa mzuri sana bi dada huyo. Aliachia tabasamu pana kwenye uso wake huku akimwangalia rafiki yake aliebaki na uso wa mashaka. " una wazimu wewe?'' Zawadi alimwambia kwa sababu hakujua kinachompa sababu ya kucheka huyo mwenda wazimu wake ni kitu gani?. Maisara alimtazama tena zawadi tabasamu la furaha likizidi kumuangazia, haraka sana alimrukia na kumkumbatia huku akiongea kwa sauti. Yaani ni kama alipiga mikelele. " Thabit kanichumbia, kanitolea posa hadi mahari tayari zawadi nahisi furaha nahisu furaha mimi, atokee mtu auone moyo wangu unavyotabasamu " zawadi alihisi furaha zaidi baada ya kusikia hilo. " Unamaanisha unachosema?" " ndio zawadi " " we kweli" alimtoa wenye kumbatio lake akaanza kumbia huku akishangiria " jamani hatimae imekuwa kweli, siamini limetia, hatimae limetimia weuweee" shangwe alilokuwa nalo zawadi lilimfanya maisara aone aibu, kwani yeye ndo alikuwa kachumbiwa lakini rafiki yake alishangiria zaidi kuliko yeye. " zawadi ni mwenda wazimu, ahahahahaa" alijikea hapo kisha akijitazama mara mbili mbili jinsi alivyo kisha akaikumbuka siku ya kwanza anakutana na Thabiti huyo mwanaume aliemchumbia. Walikuwa hostel yeye pamoja na rafiki yake zawadi wakijiandaa kutoka, siku hiyo ilikuwa siku ya ijumaa na walipanga kwenda kulala kwa rafiki yao anaeishi nje ya chuo. Mlango wa chumba chao ulisukumwa kwa kasi ya kawaida na msichana kibinge na mrefu mweupee, akaingia ndani moja kwa moja. " yaani bado tu. Nimeenda kwa white mpaka nimerudi hamjamaliza kujiandaa?" Sophie ambae ni rafiki yao wa karibu sana. " tumemaliza si unaona mwenyewe, wanafunzi wa first sijui mpoje?" Aliongea zawadi maisara akamgeukia na kumjibu. " shida sio first year shida ni wavaa miwani, ahahahaa" maisara alicheka huku wawili hao wakimwangalia kwa hasira ya kutaniana. " masikio popo wewe" zawadi alitukana. " ndo maana una komwe" Sophie nae alitia neno. " komwe linatenganisha nywele na nyusi nyie vipi?, tuondokeni mbuzi nyie" aliwaambua na kuweka begi lake mgongoni kisha wakafunga chumba chao cha hostel wakaongoza njia hadi sokoni. Sokoni walinunua mahitaji kadhaa ya usiku huo kisha wakaondoka kuelekea nyumbani kwa Sophie. " Sophie aliwahi kuchukua funguo na kufunngua mlango wa chumba chake wawili hao yeye akiwa nyuma yao walitangukia kuingia ndani. Walitupa mabegi yao hovyo na kujitupia kitandani. " hamjaja kulala hapa mbuzi nyie" Sophie aliwaambia. " sasa tufanye nini? Kwanza assignment ya madam kimei mlikusanya" alihoji maisara " ndio ulidhani tutaacha, bahati yako mimi ndo group admin kina faraja waliweka mgomo kabisa usisainiwe" zawadi alimwambia maisara alietia sura ya aibu maana hakuhudhuria muda huo kwa sababu alikuwa kalala tu hostel. " lakini si bahati mbaya kwani naonekana kuwa mzembee?" Alihoji huku akitegemea jibu kali kutoka kwa rafiki zake wawili. " bora ukae kimya" zawadi alisema na hapo maisara alipitisha kidole chake mdomoni ishara kaufunga zipu mdomo wake. Marafiki hao wa tatu walianza na ratiba zao zilizowakutanisha hapo kwa pamoja, hatimae maisara aliingia jikoni kupika chakula kitamu. Kisha wakatoka kutembea tembea wakiusogeza mda ufike. Majira ya usiku walirudi wakala na kulala zao, walikuwa wasichana fulani hivi wasio na mambo mengi, li ufupi walijitambua kitabia na walikuwa marafiki walioshibana sana. Wasio na walijaliana katika kila aina ya dhiki na hakuna ambae alitamani kuona mwenzie akikosa furaha. Majira ya asubuhi zawadi aliamka akijinyoisha nyoosha kisha akachukua ndoo akaweka maji ya kumtosha kisha akael3kea bafuni kuoga. Wakati huo maisara alikuwa tayari katoa vyombo nje anaosha, Sophie yeye alibaki kitandani kalala. " ndo maana anazidi kuwa mnene, we mtu gani analala masaa yote hayo na aridhiki?" Aliongea zawadi akizidi kwenda bafuni. Katika nyumba hiyo kulikuwa na vyumba vingi sana kama chumba cha Sophie, na bahati ni kwamba nyumba hiyo walipanga wanafunzi wa chuo zaidi hakukuwa na watu tifauti na wanafunzi, walikuwa mchanganyiko wasichana kwa wavulana. Kwa sababunilikuwa asubuhi sana basi mmoja mmoja alifungua chumba chake na kupiga mswaki, wengine wangeenda kuoga huku wengine wangeingia bafuni kwa haja zao ndogo kisha warudi kulala. Wakati maisara anaosha vyombo kwenye sink la kupigia mswaki kulikuwa na vijana wawili wakipiga mswaki, mmoja wao alikuwa mrefu mwenye mwili wa mvuto rangi yake nyeusi ilikuwa na mng'ao wa kifahari alivutia kwa hakika. Huku kando yake alisimama kijana mwenzie mwenye makamu kama yake umri miaka 27 hivi, huyu yeye alikuwa na rangi nyeupe kiasi. kwa pamoja walikuwa wakipiga mswaki huku hadithi kadhaa zikiendelea. " mpira wa jana haukuwa na mvuto kama ilivyo zoeleka, hivi chama ndo wa kushindwa kutupa heshima ule mda, yaani walikosa goal kizembe " alizungumza kijana mwenye rangi nyeupe alitambulika kwa jina la Richard. " unadhani ni rahisi kama unavyoporoja Richard, mpira so mwepesi kiasi hicho" kijana mrefu mweusi alimjibu Richard. Wakati huo aligeuz shingo yake kutazqma bombani, ndipo alipoweza kuuona uso mzuri wa maisara aliekuwa akiinuka baada ya kuosha vyombo vyote. " ni kweli usemalo Thabit, lakini kwa sasa simba inatuangusha, kuna muda natamani hadi kuhama timu, tutafakari basi tuhamie Uto ee!" Richard alimtania Thabit huku akingoja jibu kali kutoka kwa Thabit lakini Thabit alikuwa kimya. Ilibidi ageuke kusudi aone kinachomfanya Thabit awe kimya bila kuongea. Ndipo alipoweza kuona wasichana wawili wakipeana nafasi ya kuingia ndani ya chumba cha msichana aliemtambua kwa jina la Sophie maana hakuwa kazoeana nae. "Zawadi na Maisara, yupi unaemtazama kwa makini?" Ilibidi amhoji Thabit kwa sababu aligeuja jumla bila kulegeza macho, na alionekana kuvutiwa zaidi na mtu mmoja wapo kati ya hao. Kwa akili za Richard alidhani moja kwa moja Thabit itakuwa kadata na makalio yaliyofichwa ndani ya khanga ya mtoto wa kike zawadi alikuwa katokea bafuani kuoga. Maana yeye ni mwanaume alafu ashuhidie vitu kama hivyo asubuhi asubuhi. " jamaa, naona umeelewa chumbo iliyonona kwenye khanga iliyoloa eee, kumbe umo mshikaji wangu" Richard muongeaji sana alimtania Thabit. " haiwezi kuwa, nimempenda na so kumtamani, msicha aliekuwa akiosha vyombo hapo awali huyo ndo kanivutia sana" yalikuwa maneno ya Thabit kumuelekea Richard ambae aliangua tabasamu na kumjibu. " ni kweli umempenda Maisara?" " anaitwa maisara, ana jina zuri sana, kweli kabisa nimempenda na sio kumtamani" maneno ya Thabit yalimfanya Richard afikirie kuhusu kupenda, mmhh! Alikunja mdomk wake baada ya kuona hiyo itakuwa haraka sana bila shaka, hapana hataki hivyo, yeye bado muda wake kumkabidhi mtoto wa mtu moyo, huo ni muda wa yeye kula ujana. " nisaidie kunikutanisha nae" hiyo ilikuwa kauli ya Thabit kumuelekea Richard aliehisi kuchanganyikiwa. " sawa, mie tena" alijibu na kumpa Thabit tabasamu pana. Unahisi nini kitafata?????? Usikose kufatilia.......... sijawahi kuwaacha wenyewe sweetheart
Simulizi: MAISARA ( USIKU WA HARUSI YANGU) MTUNZI: KIM SWAN SIMULIZI HOUSE........... SEHEMU YA.................. 03 Hatimae wawili hao walikaa katika viti viwili vilivyokuwa vimejitenga na watu wengine kabisaa, yaani walionekana kuwa VIP kabisaa wawili hao Maisara alijawa na aibu kana kwamba hakuwa Maisara yule aliekuwa kazoeleka na Thabit kwenye simu, Thabit hakuondoa macho yake kwa kumtazama msichana huyo.mrembo aliekuwa kavaa gauni la rangi ya maziwa huku nywele zakiwa zikiwa katika muundo wa kufungwa nyuma kwa kifundo kilichofanya nyingine nining'inie. Uso wake wa mviringo ulifanya aonekane wa thamani zaidi. " kuwa huru Maisara " aliongea Thabit na hapo maisara akakaza shingo yake kana kwamba alitii amri ya kijeshi. " unataka niwe Normal, utaomba msaada kwa maneno ya mdomoni kwangu" Thabit alitabasamu, ni kweli kabisa alitamani iwe hivyo. " maneno yako yananipa faraja zaidi mimi, najikuta nakupenda tu kwa kusikia maneno yako" Maisara alihisi aibu wakati huo wahudjmu wawili waliwasili pale kwa unyenyekevu, waliuliza kitu gani ambacho wawili hao watatumia katika huo mtoko. " leta kila kilichoandaliwa hapa" aliongea Thabit Maisara akamtolea macho yake makubwa, Thabit akamuuliza. " nini?" " una sifa, kwani we muhaya" Thabit alihisi kucheka kwani kafanya nini hadi aonekane kuwa mtu wa misifa? Alafu alimuita ye muhaya? " ndio mi muhaya, alafu muhaya wa bukoba haswaa" " ahaaa! Ndo maana, usijari tumbo langu lipo free kwa kila kitu yaani mpaka hapo kaa kwa kusubiri uone mtoto wa kike ntavyokushangaza" " ahahahaa, unishangaze kwa kipi?" " ntakula kila kilicholetwa" Maisara alijibu kwa Thabit ilionekana kama Masihara lakini huo ndo ukweli alimaanisha kabisa atakula kila kitu. " kwani we unapendelea kufanya kitu gani katika maisha, nijibu japo najua unasomea sheria" " nasoma kwa sababu wanataka nisome, hata sikuwa nimechagua kitu gani nisomee ila baba tayari alifanya maamuzi nisomee sheria, kwani nani alisema anataka kuwa hakimu kama yeye?" Thabiti alimtazama kisha akajibu. " sa ntafanya nini? Sina jinsi, kikubwa nisome kwa bidii nifaulu sana na niuaminishe ulimwengu kwamba nilisoma kufaulu labda mi genius, hapana isipokua nazingatia maokoto yangu ya baadae, baba yangu ni hakimu, kaka yangu ni Hakimu pia ahahhaa, imekaaa kwa kuchekesha, lakini hiyo inanipa uhakika kabisa kwamba mimi ntapata kazi mapema mara baada tu ya kumaliza masomo yangu, najua unajua tayari connection inanilenga mimi" aliongea Maisara na kufanya Thabit acheke zaidi, ni kama aliposema ajiachie basi alfungulia bomba mvua kwa kasi ya ajabu. " yaani sijui niseme nini? Hapa nilipo nina ndoto nyingi sana, bila shaka natamani kutimiza zote, ntafungua duka la nguo za watoto, duka la urembo na kila kinachohusiana pia, subiri muda ufike nifaulu, alafu zaidi mimi napenda sana mziki, ntafungua darasa la mziki kwa ajiri ya watoto na watu wazima ili kukuza vipaji kwa wanaopenda ku dance" aliongea kana kwamba alikuwa na uwezo wakati huo. " mmhh! Una ndoto nyingi sana kipenzi, na zote unazifanya lini?" Thabit aliuliza " nikipata pesa" alijibu huku akiweka uso kwa makini. Thabit hakuweza tena kuzuia kicheko chake yaani tayari alikuwa na ndoto nyingi hivyo na alisema akipata pesa. Ahahahaa!. Wakati huo huo kila kitu kililetwa na hapo maisara alipagawa maana meza ziliandaliwa nyingi mpaka akabaki mdomo wazi. Kwani yeye aliesema atakula kila kilicholetwa alihisi ni nini? Au alikuwa amesema kwa bahati mbaya labda ulimi ulitereza? " hapana sitaweza kula hata theluthi, nipo kwenye mfungo mkali" " hapana lazima utimize ulicho ahidi, huwezi kuvunja" " sijaahidi kitu chochote mimi, zaidi ya kusema ntakula na sio ahadi usipende kusingizia watu Mungu hapendi" Thabit alihisi kumuonea huruma, haya sawa, sawa sawa, nimekuelewa mpenzi utakula kulingana na uwezo wako. Aliongea Thabit na maisara akachagua meza moja iliyokuwa imeandali vyakula mbali mbali, kwanza kabisa akalipima tumbo lake kisha akasema. " kwa hapa nahisi nusu nzima ntamaliza" hapo Thabit alimsogelea na kiti chake baada ya kuangaliana wakaanza kula kwa pamoja, " mwenyewe naona. Hivyo nusu itayosalia basi ntakula mimi hapa" kwa maneno hayo walianza kula bila kuchelewesha muda. Maisara alieahidi kula kitu hakumaliza hata robo ya chakula tayari alihisi kushiba na kumuacha Thabit akiendelea. Wakati huo huo simu yake iliingia ujumbe. [ mpenzi, mmesha agiza chakula wewe na huyo sweetheart wako, au bado unabung'aa macho unamuonea aibu] aiiii! Maisara alihisi aibu kwani alimuonaje? Aliona atapooza nini? Ngoja kwanza ajibu. [ tangu lini nikapooza mbele zake mtu? Umechundwa zawadi? Najiishi mimi sifeki mambo kwa mtu. Thabit mwenyewe yupo charming sana, nikiongea anacheka kama nini?] [ waooh waooohh waooh! Hadi nimependa hakikisha unamkamata huyo mwanaume mpaka anatangaza ndoa, nipo tayari kukusindikiza mpaka katika chumba chake usiku wenu wa kwanza] [ sitaki makando kando siku yenyewe] alijibu kana kwamba tayari aliambiwa ana pendwa? Sema alihisi uhakika ndani yake kwamba ataambiwa neno nakupenda. Hatimae walimaliza kula wawili hao na kwa pamoja wakakaa kwa utulivu kando la bwawa la kuvulia samaki. Muda wote huo maisara alikuwa akijitahidi kuvua samaki kwa uweredi ili asije kosa maana waliekeana dau kwa kila anaepata basi anaomba chochote kwa mwenzie. Bahati mbaya iliyoje kwa maisara maana Thabiti alikuwa tayari kapata mara tatu ilhali yeye akiwa amekosa kabisa. " aaaaahh! Sa ndo nini?" Alilalamika hapo na Thabit alimcheka kisha akamuuliza " umekata tamaa?" " hayo matumizi mabaya ya dhambi" " hee! Kuna dhambi nzuri" " ndio, sasa dhambi ya kukata tamaa nayo niifanye kweli hapana? Ntapambana" alijitahidi kutupia nyavu mwisho akabahatisha kumuinua samaki toka ndani ya maji akiwa bado kanasa kwenye ndoano, bila kujua alifaa amuweke nchi kavu kwanza ndo ashangirie ye kwa wenge lake alijikuta akishangiria kwa kumpata tu. " tulia utampoteza" aliongea Thabit lakini alichelewa tayari maana samaki alikuwa tayari kajinasua kwenye ndoano na amemuacha maisara. " ana roho mbaya hanipi hata nafasi ya kumshangiria" aliongea Maisara na kumuacha hoi Thabit, bila shaka ni kosa lake?. " sawa jaribu tena" maisara hakufa moyo aliamua kujaribu tena kikubwa ampate huyo samaki au samaki yeyote yule. Kwenye ndoano, mara hii alikuwa makini zaidi mpaka pale alipobahatisha kumpata huyo samaki wa kwanza kwa upande wake, Thabit alimpongeza na yeye akafurahia. " bado wa ngapi?" Thabit alimhoji baada ya kuona katimiza wawili tayari. " bado watatu nipate mkono" " sawa" Thabit hakuweza kumpinga zaidi ya kumpapu azidi kupambana, na wakati huo aliitazama saa yake na kugundua ilikuwa tayari ni saa sita za usiku. Mtoto wa kike wala hakujua kama muda umesonga. Mungu mkubwa maisara alibahatika kuvua samaki wa tano na hapo Thabit alimhoji. " umekuwa na ujuzi zaidi, vizuri sana, hutoendelea ili uridhike?" " hapana, nilisema tano acha iwe tano nimeridhika, nimepata watano wa tano for the first time, i hit it i kill it, i made it" aliongea kwa shangwe na kujikuta tayari kamrukia Thabit na kumkumbatia kwa nguvu na shangwe la kufanikiwa. " you kill me too" ( umeniua pia) aliongea Thabit na kufanya masikio ya maisara yapate utulivu, hivi kweli alikuwa akiongea na nani wakati huo? Alikuwa akiongea na Thabit ambae alijikaza haswaa kwenye mwili wake alihisi aibu alianza kujitoa pole pole huku macho yake mazuri na ya mviringo yakikosa ujasiri wa kumtazama Thabit. Unahisi nini kitafuata........?? Usikose kufatilia mkasa huu mtamuu... njoo uimalize kwa 1000 tuuuu [06/12, 17:31] +255 693 292 583: Simulizi: MAISARA ( USIKU WA HARUSI YANGU) MTUNZI: KIM SWAN TEAM: SIMULIZI HOUSE........... SEHEMU YA.................. 04 Ilipoishia............... " you kill me too" ( umeniua pia) aliongea Thabit na kufanya masikio ya maisara yapate utulivu, hivi kweli alikuwa akiongea na nani wakati huo? Alikuwa akiongea na Thabit ambae alijikaza haswaa kwenye mwili wake alihisi aibu alianza kujitoa pole pole huku macho yake mazuri na ya mviringo yakikosa ujasiri wa kumtazama Thabit. Songa nayo............ " usinionee aibu maana kila niongeacho hapa na maanisha " alisema Thabit na maisara akazidi kusogea kando na kujituliza haswaa. " Maisara , natamani sasa kuusema ukweli uliopo ndani ya moyo wangu kuanzia hivi sasa, sina mbio zaidi ya kutangaza kilichousibu moyo wangu tangu siku ya kwanza nakuona wewe hapo. Nakumiss zaidi unapokuwa mbali ama unapochelewa kujibu kila aina ya text nayo kutumia. Natamani uelewe kila angle ya neno nalo tamka toka ndani ya kinywa changu. Elewa maneno yangu ya thamani Maisara " Maisara alihisi aibu, hatimae wasaa aliokuwa akiungoja kwa hamu ulimfikia.na alijikuta useless asie na kauli yoyote ile mbele yake, ni kama aliambiwa tulia usitikise hata unyayo kusudi usikie maneno yake. " mara zote napoteza control kila ninapokuona, au unapokuwa mbele yangu. Natamani kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja huku nikijua sio sawa kwa sababu bado haujawa kamili kama mpenzi au mwanamke wangu nae muwazia. Maisara naomba uukabidhi moyo wako msafi na usio na hatia upande wangu mimi" " mimi mimi hapa sii sijui mimi hapa naomba kwanza nikae " maisara alihisi kama miguu itamuuma maana alihisi kutetemeka. Thabiti alimkamata kwa sababu alijua na kufahamu zaidi maisara ana aibu sana. " maisara " alimuita akiwa kaushika mkono wake mzuri na laini kusudi amzuie kupiga hatua, kwa ustawi na ustaarabu tayari Thabit alijikuta kaangukia goti lake moja na kumuomba akubaliwe ombi lake. Maisara alihisi aibu na kuangalia kila kona na pande za maeneo hayo ya bwawa la samaki huenda labda angeona mtu. Hapana jamani haikufaa mtu yeyote yule kuwaona. " Maisara, kama kukutongoza wewe hapo kunanipa faraja ya karne namna hii, nauona moyo wangu ukipata mlipuko wa bomu kwa kuwa kando yako, najiuliza ni vipi nitajiona mawinguni iwapo utakubali na kuwa tayari kuwa nami kando yangu, maisha yetu yatakuwa ya furaha zaidi kwa kuwa na wewe tu , kubali kunifanya wa kwako maisara, sio tu kwamba nakupenda uwe.mpenzi wangu bali nakupa ahadi ya kweli kwamba utakuwa mke wangu, nitaishi nawe daima " Thabit alitulia kidogo kisha akazungumza moja kwa moja. " Nakupenda Maisara " neno hilo moja la Nakupenda kutoka kwa Thabit lilizunguka karibu mara nane ndani ya akili na kichwa cha maisara. Maisara alizidisha aibu na kuomba apate nafasi kidogo atulie maana alihisi kupagawa kwa maneno yake tu. " Thabit naomba kwenda washroom, tafadhali " alimuaga Thabit hakuweza kupingana nae. Alielewa hali yake ya uwoga na mwisho akamwambia. " sina haja ya kupata jibu lako leo, bali nakupa wakati wako ujipe muda wa kutosha kunipenda na kuniamini " Maisara aliitikia hilo na kuondoka haraka sana kuelekea washroom. Akiwa washroom alihisi faraja, yaani alikuwa anatamani kupaa alijihisi kama angeweza angeachiwa dunia kwa muda tu ajipepee kwa furaha aliyokuwa nayo. Alifumba macho kwa aibu the way alivyokuwa akihisi. Kwani nini kilimkuta jamani loo! Yote hayo kwa sababu tu ya kutamkiwa maneno ya kupendwa tu. Loo! Baada ya kujichangamsha huko washroom hatimae alipunguza aibu kwa kila neno la ujasiri alilojipa kisha akatembea moja kwa moja mpaka alipomuacha Thabit. Thabit alimshika mkono wake na kwa pamoja waliongozana mpaka kwenye gari. Hawakuwa na haja ya kusubiri hapo kwani muda ulikuwa umeenda sana. Kwenye gari maisara alikuwa kimya kwa aibu sana kiasi kwamba Thabit alihisi kuwa bored. " niwashe mziki?" Thabit alimhoji maisara " ndio washa" maisara alikubali kwa sauti ya pekee ambayo ilimfanya Thabit achanganyikiwe, kumbe kuna muda alikuwa na sauti ya utulivu sana. Alitabasamu na kuwasha mziki ambao ulianza kumpa hamasa ya kuusikiliza zaidi. Wakati huo gari ilikuwa imeenda sana kiasi kwamba alikaribia hadi kufika hostel. ♧ Just a smile and rain is gone♧ ♧can hardly believe it yeah ♧ ♧ There's an angel standing next to me ♧ ♧ Reaching for my heart ❤ ♧ ♧ just a smile and there's a no way back♧ ♧ can hardly believe it, yeah♧ ♧ But there's an angel calling me♧ ♧ Reaching for my heart ❤ ♧ ♧ i know that I'll be okay now ♧ ♧ This time it's really ♧ ♧ I lay my love on you, it's all i wanna do, every time i breathe, I feel brand new♧ ♧ you open up my heart ❤ ♧ ♧ show me all you'll have♧ ♧ and walk right through ♧ ♧as i lay my love on you♧ Hatimae kwa wakati huo ambao ndo gari iliwasili katika hostel maisara alikuwa kazama katika hisia za wimbo mtamu ambao alihisi kabisa Thabit aliuweka kwa ajiri yake ama kwa sababu yake mwenyewe. Alihisi faraja baada ya kufunguliwa mlango na Thabit, akampa.nafasi ya kutembea huku wimbo ule ule ukiendelea. Wimbo ulimaanisha. ♧ Tabasamu tu na mvua imeisha, ni ngumu sana kuamini, kweli,, kuna malaika kasimama kando yangu, kuufikia moyo wangu,, Kwa tabasamu tu, sina njia ya kurudi nyuma, ni ngumu kuamini, kweli, lakini kuna malaika ananiita,, kuufikia moyo wangu♧ ♧lakini najua ntakuwa poa sasa, muda huu ni ya ukweli♧ ♧ nayaweka mapenzi yangu kwako, ndo nachopenda kufanya, muda wote naopumua, najihisi kuwa mpya,, umeufungua moyo wangu, nionyeshe kila utakacho, na upite ndani yake. Kama nilivyolaza mapenzi yangu kwako♧ Maisara alitabasamu baada ya kuangaliana na Thabit kisha akakosa neno. " ufike salama sawa" Thabit alimsemehsa. " mmhh! Sawa nawe ufike salama, uendeshe kwa makini barabarani " maisara hatimae aliongea sauti ndefu baada ya dakika nyingi kukatika. Thabit alitabasamu na kumkumbatia kiasi huyo msichana mrembo aliekuwa kasimama mbele yake. " kwa heri, Nakupenda sana" alimwambia kisha akambusu kidogo kwenye paji la uso wake. Maisara alitembea taratibu akiwaza kila kilichojiri siku hiyo, aiii! Ilikuwa super alitamani muda urudi nyuma aambiwe maneno yale aliyoambiwa na Thabit. Aliingia ndani baada ya kukuta tayari wambea wawili ambao ni Zawadi na Sophie washamfungulia mlango huku wakisubiri kujua kilichojiri. Maisara alipagawa kiasi cha kushindwa kuona uwepo wao. Unahisi nini kitafuata........?? Usikose kufatilia mkasa huu mtamuu... PATA OFAA YA LEO TUU....... Simulizi: MAISARA ( USIKU WA HARUSI YANGU) Chombezotu.blogspot.com SEHEMU YA.................. 05 Ilipoishia............... Aliingia ndani baada ya kukuta tayari wambea wawili ambao ni Zawadi na Sophie washamfungulia mlango huku wakisubiri kujua kilichojiri. Maisara alipagawa kiasi cha kushindwa kuona uwepo wao. Songa nayo.................. " tuelezee basi nini kilijiri?" Zawadi alishindwa kuvumilia ilibidi amshtue huyo mwanamke amsimulie kwa nini alikuwa na furaha kubwa kiasi hicho. " jamani wewe Maisara tusimlie sisi" Walianza kurejea maneno hayo mpaka Maisara akahisi kuwakatia tamaa kwa nini hawakumpa muda wa kumuwaza Thabit wake. " twambie wenzio tuna arosto ya kujua kila kitu sema basi" " eeehh! Nasema bhana nyie vipi?" Aliwapigia kelele wakawa kimya kisha akaongea taratibu. " ki ufupi, ameniambia ukweli nilioufata siku ya leo, lakini mimi nimeshindwa kumpa jibu nililoandaa kwa ajiri yake tangu mwanzo" " weeeehh!" Zawadi alikaa karibu zaidi akihisi labda itakuwa ngumu sana kumsikia Maisara, Maisara alianza kuhadithia kila kitu mpaka akarejeshwa hapo nyumbani, Zawadi alijikuta kashika tama akimuonea raha rafiki yake jamani huyu msichana mrembo kapata bahati kiasi gani? Alijawa hisia kiasi kwamba uso.wake uliwaka kwa hisia na kuwa mwekundu kama nyanya. Hakuchelewa kumrukia na kumkumbatia. " nakuombea awe mtu muelewa na mzuri zaidi milele jamani, I feel proud of youu sweetheart" Sophie pia aliungana na kumbatio la wawili hao huku wakimuombea asiwe muoga wakati mwingine aseme tu anampenda pia huyo mwamba. Maisara alikubaliana nao wenzake. Siku hiyo ilipita na siku zikasonga huku Maisara akizidi kuwa karibu na Thabit, hatimae Thabit alimaliza masomo yake kwani hakuwa akisoma tu bali alikuwa akisoma kwa sababu zake mwenyewe binafsi, kama ni kuhitimu alihitimu tayari hapo awali. Maisara alikuwa mwaka wa pili siku ambayo aliweza kumkubalia Thabit na kuthibitisha moyo wake kumpenda moja kwa moja. Siku hiyo ilikuwa siku ambayo wanafunzi waliomaliza pamoja na Thabit wakifanya mahafali ya graduation, lakini kwake yeye Thabit hakuwa tayari kufanya mahafali, hivyo alichukua cheti chake tu na kuondoka zake bila hata kupiga picha. " sasa kwa nini hajafanya mahafali, nilitegemea atakuja na siku hii special kwake niifanye iwe special zaidi lakini ameishia kuondoka bila hata kusema chochote " alilalamika Maisara kwa sababu alimuandalia surprise pendwa Thabit na alipanga kuudhihirisha moyo wake siku hiyo. " ni sawa kama mambo yameenda tofauti na ulivyopanga lakini sasa nii unaweza kumpatia surprise hii kwa muda wa pekee yenu, kwa nini usimwambie mkutane mahali ili umpe zawadi ulioandaa kwa juhudi kubwa" Zawadi alimwambia Maisara akabaki hana usemi alinuna tu. Akiwa kavimbisha mashavu yake simu yake iliita " My heartbeat" jina lilisomeka namna hiyo kwenye kioo cha simu yake. " amepiga pokea" Sophie alimpa simu haraka.sana Maisara alipokea pia. " halo" alianza kwa kuongea " samahani sweet, nimeondoka kimya bila kukutaarifu mpenzi wangu" " sawa tu" " samahani, naomba nijipe muda kwanzia saa hii jioni mpaka kesho asubuhi kwa ajili yako, iwapo kuna chochote ulitamani kuongea na mimi au ulitaka nipatia ni muda wako sasa" " nilitaka kuongea na wewe zaidi, sina zawadi zaidi ya maneno tu" maisara aliongea. " nayatamani hayo hayo ya thamani " alisema Thabit na wakati huo huo maisara hakuchelewa kumpa maelekezo wapi wakutane. Na ndo hiyo siku ambayo alifanikiwa kukiri maneno matatu muhimu ya kiingereza mbele ya upeo wa uso wake. Alimpatia box dogo la zawadi kabla ya yote kisha akamuomba afungue. Thabit alifungua na kukutana na karatasi nyeupe kabisa isiyo na maneno yoyote yale. Aliutazama uso wa Maisara akatamani kuuliza mbona karatasi tupu? " ondoa hiyo" maisara alimwambia kwa ishara na hapo Thabit aliondoa na kukutana na karatasi nyekundu ikiwa imeandikwa kwa wino pendwa wa rangi nyeupe. " I" ilisomeka herufi hiyo kwa wino uliokorea na kwa harufi kubwa. Kisha alitoa karatasi hiyo na kukutana na karatsi nyeusi iliyokolezwa na maneno meupe. " need your permission" alisoma karatasi hiyo pia kisha akatoa na kuendelea kufunua karatasi zaidi karatasi iliyofata ilisomeka kwa maneno meupe pia " to confess my feelings " hapo Thabit aliweza kuachia tabasamu lake baada ya kuona ndani ya box hilo dogo hakuna tena karatasi zaidi. " I need your permission, to confess my feelings" ( nahitaji ruhusa yako kukiri hisia zangu) alisoma kwa pamoja Thabit. " ndio namaanisha Thabit " alizungumza Maisara kisha akasogea karibu yake sana alimkumbatia Thabit bila aibu japo ndani kabisa ya moyo wake alihisi kulia na kutamani kujificha. " Thabit " aliita jina lake kisha akamwambia. " Muda umefanya nielewe, kukuchagua wewe ni chaguo bora zaidi la maamuzi niliyowahi kuyafanya hapo awali katika maisha yangu. "Najua imekuwa ngumu kuelewa moyo wangu unataka nini lakini umekuwa mwepesi zaidi kuzielewa hisia zangu, ni ukweli uliowazi kwamba nakupenda zaidi wewe, ni ukweli sitaficha tena hisia hizi zisizoeleweka Thabit, Nakupenda sana hivi sasa" Thabit alihisi raha sana, ni vile tu Maisara hakuwa na ruhusa ya kuuvamia moyo.wa Thabit ili ajue kuna kipi ndani yake kweli Thabit alihisi ushindi usiopingwa ndani yake, hatimae sasa alikuwa na ruhusa ya kufanya maamuzi mengi juu yake japo hakuwa na haki ya kumfanya mke wake. Lakini angalau alikuwa na nafasi ya kuibusu kwa muda mrefu midomo yake mizuri sana. " ndio Thabit, Nakupenda na natamaninuwe wa kwangu, sijui ni vipi uliweza kunipenda mimi lakini kujari na kusumbua kwako hapo awali kulifanya nikupende zaidi" Thabit alimshika chini ya mashavu yake na mikono yake miwili kisha akambusu midomk hake mitamu, Maisara alitulia japo ilikuwa kwa kushtukiza lakini ilikuwa kana kwamba alijiandaa kwa hiyo busu. " Nakupenda zaidi maisara " aliongea Thabit na kumfanya Maisara ajae raha na gabasamu kwenye uso wake. Usiku huo walipata muda wa kuongea mambo mengi sana na zaidi wakipanga mustakabali wao vipi uende. Thabit alimwambia kama ilivyo yeye kampa jibu katika siku yake hiyo ya graduation basi na yeye pia atamshangaza sana katika siku yake ya graduation, kitu pekee anachofaa kufanya ni kusoma kwa bidii na kuhakikisha hafanyi makosa katika maisha haya ya chuoni, anafaa kusoma kwa bidii ili kusudi hapo baadae aweze kutimiza ndoto zake alizomuahidi hapo awali. " bila shaka nitafanya hivyo Thabit nitafanya kila kitu kwa ajiri ya future yetu" alimpa ahadi ya kusoma kwa bidii na kutimiza kila kitu kwa bidii. Na hapo ndo muda ambao Thabit alimwambia atamsapoti.kwa kila jema lake. Unahisi nini kitafuata........?? Usikose kufatilia mkasa huu mtamuu...

Smartwatchs

Post a Comment

TOA MAONI YAKO HAPA

Mpya zaidi Nzee zaidi