NILIEMDHANIA KAHABA KUMBE NI BIKRA

.

29 - 30 MWISHO SEASON ONE

.

NILIEMDHANIA KAHABA KUMBE NI BIKRA

.

SURA YA ISHIRINI NA TISA

.

Roma hakuwa ni mwenye kujali sana kuhusu maneno ya Edna kwani muda huo alichokuwa anawaza ni kiwanja gani anaweza kwenda kula bata , na angalau kujipatia kitumbua ambacho kinaweza kumtuliza kwa siku hio ya Wikiend.

.

Wakati akiwa anaingia kwenye Daraja la Kigambomi kuna gari aliitilia mashaka kwani hisia zake zilimwambia kabisa gari hio ilikuwa ikimfatilia , lakini licha ya kuwa na hisia hizo alitamani kulithibitisha hilo na ndio maanba alianza kuchukua chocho ambazo zilikuja kumfikisha mtaa wa Chang`ombe , lakini Gari ile bado ilikuwa nyuma yake.

.

“Kuna wapuuzi wananifatilia”Aliwaza Roma huku akiendelea kukumbuka kuwa gari ile ilikuwa karibu na nyumba anayoishi na kwa namna yoyote ile ni kwamba watu hao wanataarifa la eneo ambalo anaishi nah ii aliona ni hatari kwa yeye na kwa familia yake yaani Bi Wema na Edna.

.

“Ngoja kwanza niwapoteze “Aliwaza huku akiongeza spidi ya gari na muda huu magari yalikuwa mengi barabarani kwani ilikuwa ni muda wa jioni jioni hivi watu wakirejea majumbani , lakini licha ya magari hayo mengi haikumsumbua

.

Roma kuendesha gari kwa spidi na kuanza kupita kila apatapo nafasi na alitumia dakika chache tu gari iliokuwa inamfatilia alikuwa ameipoteza , lakini sasa alijishgaa kuona ameendesha gari umbali mrefu mpaka kufika Kawe. “Bora niende zangu Beach”Aliwaza Roma na kuendesha gari kuelekea upande ilipo kuwepo Ufukwe wa Kawe. Wakati anaingiza gari yake eneo maalumu la kuegeshea magari wapo watu wengi waliokuwa wakimkodolea macho kutokana na uzuri wa gari yake.

.

“Bosi kuna boti zipo hapa kama utahitaji”Aliongea kijana flani mara baada ya kumuona Roma akitoka kwenye gari, kijana huyo alionekana kuvaa tisheti flani hivi ya kampuni iliokuwa imeanzishwa hivi karibuni ndani ya jiji la Dar es salaam ambayo ilikuwa ikikodisha SpeedBoat , boti flani hivi zipo kama pikipiki.

.

Roma alijikuta akitamani kweli kuendesha boti na aliongozana na kijana yule mpaka upande ambao Boti hizi hukodishwa.

.

Baada ya kufanya malipo ya awali , alionyeshwa upande ambao boti hizo zilikuwa zimeegeshwa na Roma alisogea upande huo na kuchagua boti ambayo ilimvutia na alionekana alikuwa akijua kweli boti hizo.

.

Baada ya kuridhika na chaguo lake alirudi na kubadilisha nguo na kupewa mavazi ya ziada kwani hakuwa na mpango wa kuja ufukweni hivyo hakuwa na nguo za fukwe. Siku hii ndani ya eneo la fukwe kulikuwa kumechangamka mno kiasi kwamba kulikuwa kumependeza , kuna waliokuwa wachumba wakiwa ndani ya hili eneo , kuna waliokuwa ndani ya fukwe hii kama wanafamilia na pia kuna waliokuwa wapo ndani ya fukwe hii wakiwa peke yao kubarizi.

.

Roma hakujali sana juu ya watu hao, ila kwake muda huo ni kufurahia maji ya baharini kwa kutumia speedboat. Upande mwingine kwenye maegesho ya

.

magari , iliingia gari aina ya Nissani nyeusi na kupaki pembeni ya gari ya Roma na wakashuka mwanamke mmoja wa kizungu pamoja na mwanaume wa kizungu , wote wakiwa wamevalia Track suit pamoa na tisheti

.

, baada ya kushuka waliangalia gari ya Roma na kisha wakatingishiana vichwa kama ishara na kisha walisogea upande wa fukwe.

.

Baada ya kufika kwenye fukwe walianza kuangaza macho yao kulia na kushoto kama watu waliokuwa wakitafuta jambo Fulani na ndani ya dakika kama mbili hivi walijikuta wakipeana ishara mara baada ya kuona boti iliokuwa kwenye spidi ikipotelea katikati ya maji.

.

Ni kitendo cha haraka sana mzungu yule wa kike alirudi kwenye gari na kutoa begi flani dogo na kisha kutoka na kuungana na mzungu wa kiume na kuelekea kwenye kampuni ambayo ilikuwa ikikodisha Speedboat na kulipia moja na dakika chache tu walionekana wakiwa kwenye boti ile huku wakiitoa kwa spidi kiasi kwamba watu walianza kushangaa kwa umahili wao. Na kwa jinsi walivyokuwa wanaonekana kama ungewaangalia ungesema watu hao watakuwa ni wapenzi kwa namna yoyote ile ,kwani walikuwa wamependezana.

.

Roma alikuwa akiendesha mdogo mdogo huku akiwa ni mwenye kufurahia upepo uliokuwa ukimpepea machon kiasi cha kumpelekea kufumba macho.

.

“Hey! Bro , ilisikika sauti iliomwita Roma akiwa katikati ya maji kiasi cha kufumbua macho , kwani muda wote alikuwa ameyafunga akifurahia upepo, Na Romaa baada ya kugeuza macho yake alimuona msichana mrembo akiwa kwenye boat kama yake , alikuwa ni mrembo haswa kiasi kwamba Roma pepo la ngono liliibuka hapo hapo

.

Kimakadirio mwanamke aliekuwa mbele yake alikuwa mdogo sana kiumri kati ya miaka ishirini hivi kushuka na Roma alimkadiria mwanadada huyo kama mwanafunzi wa chuo kama tu atakuwa anasoma. “Mambo mrembo?” “Poa! Tunaweza kushindana?” “Kushindana kufanya nini?” “Kuendesha”Hapo Roma alimuelewa na kisha akatabasamu. “Hautoweza kunishinda wewe” “Hata mimi hautoweza kunishinda”Aliongea Mrembo na wote hawa wawili licha ya kwamba walikuwa wamekaribiana na boti zao ,lakini walikuwa wakuiongea kwa sauiti kubwa ili kusikilizana kwani upepo ulikuwa mkali kiasi kwamba sauti ilikuwa ikipotea. “Sawa lakini lazima kuwe na zawadi kwa mshindi , ukiweza kunishinda nakupatia gari yangu niliokuja nayo”Aliongea Roma. “Gari aina gani umekuja nayo ambayo unaamini ninaweza kuikubali kama sehemu ya zawadi kwa mshindi?” “Aud Q8”Aliongea roma na kumfanya mwanadada huyu atabasamu kwani gari hio alikuwa akiijua vyema ugharama wake katika soko la magari duniani , ni gari ambayo sio chini ya milioni 200.

.

“Mimi ukiweza kunishinda nakupa mwili wangu leo?”Aliongea yule mwanadada kwa kujiamini na kumfanya Roma acheke.

.

“Hehe.. unaonekana unajiamini sana mremb?,o kumbuka kutimiza ahadi ” “Ndio hakuna ambaye ashawahi kunishinda kwenye mbio za baharini , nina medali nyingi nilizopata chuoni” “Chuo gani unasomea?” “Yale university”Aliongea manadada huyu na kumfanya Roma atabasamu . “Okey ! deal ule wako uende kinyume na ahadi yako” “Siwezi kwenda kinyume na ahadi yangu ni moja ya sharia nilizojiwekea”

.

“Karembo sana haka nitahakikisha nashinda nikakavue nguo nione kamebeba nini?”Aliwaza Roma huku wakijiandaa kuanza mtanange na kuamua mstari wa ushindi , mwanadada huyu mrembo ambaye jina bado hatumjua alionekana kujiamini mno. “Ukute anafurahi mwenyewe atanishinda Looh! yaani nikuvulie nguo mimi”Aliwaza mrembo huyu na muda huo huo wakaanza kuendesha kwa spidi huku membo huyu akionekana kuwa imara kweli , kwani ni ndani ya dakika moja tu alikuwa amemuacha mbali kidogo Roma , lakini kwa Rroma hakuwa na wasiwasi hata kidogo ,alikuwa akiendesha kama hataki vile. Mwanadada aliekuwa mbele , alionekana kumdharau Roma na kuona hakuwa saizi yake , lakini ghafla wakati akiendelea na mawazo hayo , alipitwa na Roma kwa spidi ambayo haikuwa ya kawaida na kumfanya mrembo huyu ashangae na kuanza kuongeza Spidi, kwani Roma alikuwa ashamuacha hatua kadhaa mbele.

.

“Shi**t Atanishinda huyu”Aliongea huku akiichochea boti yake na ikaanza kusererka kiasi kwamba kulionekana povu la maji ya baharini likiwa limejitengeneza kwa nyuma. Mchezo huu walikuwa wamewekeana umbali ambao walitakiwa kufika , kwa mbele kabisa kulionekana kukiwa na mnara ambao ndio

.

mwanadada huyu alipendekeza , japo ilikuwa katikati ya bahari kwenye maji mengi ila hawakuongopa , lakini sasa , kadri alivyokuwa akijitahidi kuendesha hakuwa akimfikia Roma na hapa akili yake ilianza kupata moto na kujiuliza huyu mtu ni wa namna gani kwani katika Maisha yake yote hajawahi kushindwa kwenye mchezo huo na anazo medali.

.

Mwanadada huyu mrembo alianza kujutia maamuzi ya kuuweka mwili wake Rehani aliona kabisa dalili za kuliwa zinaenda kutimia.

.

Roma na yeye hakuwa na utani kabisa mbele ya kitumbua , alihakikisha anashinda na hilo alilikuwa akikaribia kulifanikisha kwani alikuwa akikaribia eneo ambalo ndio mstari wa ushindi. Mrembo huyu alijikuta macho yakimtoka mara baada ya kumuona mwamba Roma akipita mnara kwa spidi na kuwa mshindi.

.

“Shi**t nishaliwa leo”Aliongea huku akipunguza mwendo lakini ghafla alimuona Roma akipiga kona ya hatari sana kuzunguka mnara ule na kuja upande ambao yupo kwa spidi ya

.

hali ya juu sana kiasi kwamba mwanadada huyu alianza kujawa na hofu na kujiuliza ni kitu gani mwanaume huyu asiemjua anafanya , lakini alikuja kujua baada ya dakika chache , kwani ile Roma anamfikia yule mrembo aliisukuma bot ya yule mrembo kwa kutumia boat yake kwa nguvu na kuacha uwazi na hapo hapo ikapita Boat nyinngine sehemu ambayo boti ya mrembo yule alikuwa ameisimamisha na ikawa ponea ya mrembo huyu.

.

“Pumbavu wana siraha”Aliongea Roma baada ya kuona mwanadada wa kizungu kutoa bundiki yake kubwa na kumlenga , yule mrembo mwanzoni hakuwa akielewa kinachoendelea ila alipoangalia kwa umakini aliona bunduki na kuanza kupatwa na hofu na kujiambia leo anakufa katikati ya bahari , na eneo walilokuwepo ni kama vile watu hawa walikuwa wakiwasubiria waende mbali ili kuanza kuwashambulia wakina Roma kwani ilikuw ani mbali na fukwe.

.

Roma aliona yule mzungu akivuta Triga , lakini hakutaka kufa kizembe , aliipindisha Boti ile kwa upande mmoja wa kulia ina ikainama kiasi ambacho bega la Roma liligusa maji huku yeye akiinama na kichwa pia kugusa maji na boti ile kubinuka upande mmoja na kilichosikika hapo ni risasi mbili mfululizo zilizotua upande wa chini kabisa wa Boti.

.

Kwa jinsi Roma alivyokinga risasi ile kwa Boti ni kitendo ambacho mrembo aliekuwa pembeni hakuwahi kukishuhudia katika Maisha yake aliona kama yupo kwenye muvi.

.

Mzungu yule wa kike alishindwa kumlenga Roma kwani hakuwa akimuona kwa upande ambao walikuwa wapo

.

,kwa kitendo cha boti ya Roma kubinuka upande na nikama Roma alikuwa akifanya makusudi , baada ya wao kuona Roma amejiwekea kinga kwa kutumia boti ile , waligeuza kwa spidi kwenda upande mwingine na hapo mrembo yule alijikuta akizidi kupagawa , lakini alikuja kupiga mshangao mara ya boti ya Roma kurudi katika usawa wake , lakini kwenye boti hakukuwa na mtu na hata wale wazungu walishangaa kwa wakati mmoja na kujiuliza ni kitu gani kimetokea , walionekana kuhaha.

.

Umbali ambao Roma alikuwa amesimama na umbali ambao wazungu walikuwa wamesimama ilikuwa mita kama ishirini hivi. Mrembo yule alikuwa kwenye hali ya mshangao na alijiambia huenda mwanaume yule Kazama chin na Risasi ile imempata ., hakutaka kujiuliza mara mbilimbili na yeye alijitupa ndani ya bahari huku akidhamiliia kufanya jambo la kiuokozi. Huku nje wale wazungu walishangazwa na tukio hilo , lakini pia na wao walidhania mtu aliekuwa wakimshambulia atakuwa Kazama , lakini haikuwa hivyo kwani ile wanapunguza spidi ya boti yao kulitokea tukio kama la Dolpin kuruka sarakasi kwa kutokezea nje ya maji na yule mwanamke alivutwa kwa kushikwa kwenye mkono kwa nguvu na kuachia libunduki lake na baada ya kuvutwa alizamishwa kwenye maji na kukatulia tuli.

.

Wakati hayo yakiendelea mrembo yule mwingine alikuwa akitokelezea kwenye maji huku akionekana kuvuta pumzi na kurudi tena kupiga mbizi , huku akiacha kuangalia upande walikokuwa wale wazungu aliowaacha , alirudi tena ndani ya maji kwa ajili ya kumtafuta Roma .

.

Yule mzungu aliekuwa amebakia baada ya kuona tukio lile na yeye alijitosa katika maji, huku akiwa amevalia miwani ambayo ilionesha kumsaidia kuona akiwa ndani ya maji kama anavyokuwa nje , na hapo ndipo aliposhuhudia jambo la kutisha kabisa kwani alishuhudia Roma akiwa amemzamisha mwenzake chini kabisa ya maji. Kina ambacho hata yeye mwenywe hakuwa na ujasiri wa kwenda , kwani walikuwa wamegusa eneo la sakafu kwenye mawe . Mzungu yule alimuona Roma akimvunja shingo mwenzake na aliishia kutoa kilio . “Noo ..Nancy “wakati amepanua mdogo kumuita mwenzake , Roma alipanda kama mshale au unaweza kusema kama zile roketi zinazoenda masafa ya juu na ni kitendo cha kufumba macho na kufumbua Roma alimfikia yule mzungu na kwakua mzungu yule hakuwa kwenye kujiandaa kutokana na kushuduhudia tukio la mwenzake kuvunjwa

.

shingo. Alijikuta ameshikwa na yeye kwa staili ya Roba shingoni na kuzamishwa chini ya maji . Upande wa huku nje mrembo ambaye alionekana kuwa jasiri licha ya kuona bunduki na majambazi yale ya kizungu ambayo yalikuwa yanamshambulia Roma alitokezea nje tena , lakinni awamu hii akiwa amekata tamaa kwani alikuwa amemkosa Roma

.

chini , lakini ile anaangalia upande wa wale wazungu hakuona mtu kwenye ile boti na kushangaa Zaidi , wakati akiendela kushangaa , aliaona mtu akitokezea kama samaki ma kuvuta boti na kuketi huku akiwa anavuja maji mwilini

.

Yule mrembo alipanda kwenye boti huku akiwa ni mwenye kushangaa na akiendelea kutafuta wale wazungu wamepotelea wapi , lakini hakuwaona . “Vipi mrembo , mbona unashangaa hivyo”Aliongea Roma kama kawaida yake

.

utadhani hakukuwa na tukio lililokuwa limetokea Yule mwanamke bado alionekana kuwa nah ofu , alikuwa akiangalia ili wawaone wale wazungu , lakini kwake ni kama walikuwa wamepotea na alikuwa haamini kama wale wazungu wamepotea maana ni ghafla sana. “Unaitwa nani mrembo?”Aliuliza Roma na kumfanya yule mwanadada amwangalie Roma kwa mshangao.

.

“Naitwa Donyi”Aliongea mwanadada huyu na Roma akatabasamu. “Sasa Donyi nadhani ni muda wa kutawaza mshindi na mwenye kupata zawadi yake apate” SEHEMU YA THERATHINI Baada ya Roma na Donyi kurudi tu nchi kavu , mara vijana waliokuwa wamevalia Suti walikuja na kumzunguka Donyi , kitendo ambacho kilimuuzi sana Donyi kwani hakupenda walinzi ambao walikuwa wameajiriwa na baba yake kwa aili ya kumilinda.

.

Alimgeukia Roma huku walinzi wale wakimwangalia Roma kwa macho ya utahadhari , lakini kwa upande wa Roma kwanza hakushangaa sana

.

, maana baada ya kukumbuka kwamba msichana huyo alimwambia kuwa anasoma chuo cha Yale , chuo ambacho licha ya ada yake kuwa kubwa lakini pia sio wanafunzi wote kutoka mataifa ya Afrika wanaweza kusoma ndani ya chuo hiko na hilo kwa Roma ilikuwa ishara tosha kwamba Donyi familia yake haikuwa ya kawaida ndani ya taifa hili la Tanzania.

.

“Siku nyingine Mungu akitukutanisha nitatimiza ahadi yangu”Aliongea Donyi na Roma alitabasamu na wakagana , ukweli ni kwamba Roma hakuwa na mpango wa kulala na mrembo huyo hakuelewa ni kwanini lakini hakuwa na msukumo wa aina yoyote wa kufanya nae mapenzi.

.

Muda umekuwa umeenda na Roma hakuwa na mpango wa kukaa sana nje ya nyumbani kwa siku ya leo , aliwaza kwenda nyumbani akapumzike. Masaa machache tu alikuwa ashafika na kuingiza gari yake ndani, lakini aliona gari mpya ndani ya eneo la kuegesha magari kwa muda na aliona lazima kutakuwa na ugeni , lakini bado alijiuliza ni nani kafika nyumbani kwake muda huu wa jioni ya saa kumi na mbili.

.

Kama alivyohisia kuwa kuna mgeni , ni kweli aliona mwanaume ambaye hakuwa akimjua akiwa ameketi kwenye masofa , uwepo wa huyu mwanaume haukumchanganya sana wala kumshangaza , kilichomshangaza ni kwamba Edna alionekana kucheka kweli mbele ya huyu mwanaume na alijiuliza ni ukaribu gani mwanaume huyu anao na mke wake. Roma karoho ka wivu kalianza kumuingia , kwani licha ya kwamba zilikuwa ni siku chache tokea aanza kuishi na Edna hakuwahi kumuona mwanadada huyo akifurahia namna hio. “My Beutifull wife nimerudi”Aliongea Roma na kisha alienda moja kwa moja upande ambao alikuwa amekaa Edna na kisha akambusu shavuni , Edna alitamani amkwepe Roma lakini alishindwa kufanya hivyo kwani kulikuwa na mgeni.

.

“Mke wangu hujanitambulisha kwa mgeni na wala haujaniambia kuwa tunatembelewa leo”. “Elvice huyu ni mume wangu , anaitwa Roma , Roma huyu ni Rafiki yangu wa utotoni mpaka ukubwani anaitwa Elvice ni mwanajeshi lakini pia ni rubani”Aliongea Edna kwa kuchangamka , lakini muda wote bwana huyu mgeni mwenye sura ya kihandsome , anaejipenda kutokana na mavazi yake , alionekana muda wote kumuangalia Roma pasipo kummaliza, ni kama alikuwa akimlinganisha na Edna na kujiuliza imekuwaje Edna akaolewa na mtu wa kawaida kama Roma.

.

“Nafurahi kukufahamu Elvice ,japo sijapenda uzuru wa usiku usiku nyumbani kwangu”Aliongea Roma na Edna aliekuwa karibu na Roma kwenye sofa alimfinya, ila Roma hakujitingisha wala kuonesha dalili za maumivu. “Nafurahi na mimi kukutana na wewe Roma , nimekuwa ni wakujiuliza ni mwanaume wa aina gani kaweza kuutingisha moyo wa Edna, nadhani sasa nina majibu”Aliongea Elvice . “Roma Elvice alikuwa akinisimulia habari za Jeshini , hapa nimejikuta nikicheka hatari , zinachekesha kwakweli ,Elvice hebu tuendelee na hio stori basi”Aliongea Edna huku leo akionekana ni mwenye kuchangamka sana kuliko siku zote. Elvice aliendelea na stori huku Roma akiwa pembeni akisikiliza hio stori ambayo imemfanya mke waka afurahi , lakini kadri Elvice alivyokuwa akiendelea kusimulia , Roma aliona ni uongo mtupu. “Acha kumdanganya mke wangu”Aliongea Roma huku akionesha hasira sana. “Unamaanisha nini nadanganya , ushawahi kufika jeshi wewe,Nikuambie tu Mr Roma ukkama ungepewa kikosi kama nilichopewa mimi ukiongoze na ukakutana na kipigo ungejikojolea”Aliongea Elvice lakini kwa Roma maneno yale yalionekana kama kejeli. “Unaongea upumbavu , unaongea mambo ambayo hayana uhalisia hata kidogo na ole wako uendelee kumdanganya mke wangu uone”Aliongea Roma kwa msisitizo lakini Elvis alionekana kuendelea , swala hilo lililimfanya Roma ahisi kichwa kuuma sana na kuanza kuona pichapicha za miili ya watu ikiwa imekufa ikiwa imemzunguka huku yeye mikono yote akiwa na damu. Ni kama vile muvi ilikuwa ikipelekwa mbele kwa namna ambavyo Roma alianza kuona mapicha picha hayo , maumivu ya kichwa yalikuwa makali kiasi kwamba aling`ata meno na kuinama , lakini Elvice aliendelea kusimulia , kila neno ambalo Elvice alikuwa akiongea ni kama lilikuwa live kwenye kichwa cha Roma . Elvic na Edna hawakujua kinachoendelea kwani Roma macho yalikuwa yashabadilika Rangi na kuwa ya kijani huku yakiwa yametengeneza aina flani ya mishirizi ya damu.. lilikuw ni picha ya lutisha Ilikuwa ni kitendo cha haraka sana Elvice alijikuta akining`inia hewani huku akianza kukohoa mfuliulizo , huku Roma akiwa amemshikilia kwa mkono mmoja. “Nikikuambia acha acha , kwangu onyo ni mara moja tu”Ni sauti kama ya Roboti iliokuwa ikisikika Sebuleni hapa na kumfanya Edna atetemeke , alimuona kabisa Roma akiwa amebadilika macho , na leo hii kwake ni kama ilikuwa mara ya kwanza kumshuhudia Roma rangi ya mboni za macho yake kuwa za kijani , mrembo huyu alitetemeka , lakini kwa Elvice alionekana ni kama mtu aliekuwa akinyongwa na Kamba kwenye shingo kwani alikuwa akitapatapa kwa kurusha miguu kukata roho huku Roma akionesha hana ishara kabisa ya kumuachoa na alionekana alikuwa akishindwa kuutawala mwili wake kabisa , kwani muda hio alionekana kama mnyama ambae mbele yake kulikuwa na kitoeo

.

Ilikuwa ni kitendo cha kijasiri sana alichokifanya Edna , alimsogelea Roma kwa nyuma na kumkumbatia akipitisha mikono kwa mbele.. “Roma Please

.

Stop….”Aliongea Edna huku akitoa machozi na ni kama vile Roma alichomwa na sindano kwani alimwachia Elvice akadondoka chini na kisha akageuka nyuma na kumwangalia Edna anavyolia na ilichukua sekunde chache tu Roma alidondoka chini na kuzimia. “Romaaa… Romaa !!!”Ilikuwa ni kama ndoto iliokuwa ikiendelea katika kichwa cha Roma , kwani alijiona akiwa yupo katikati ya msitu mnene huku akimwangalia mwanamke aambaye alikuwa amefanana kwa kila kitu kama Edna akimkimbilia huku akiliita nina lake , na hii yote ni

.

baada ya Roma kupigwa risasi ambazo zilitua kwenye kifua chake,Risasi ambazo zilimpiga mfululizo , lakini wakati mwanamke yule akimkimbilia , mara aliona watu wale wale waliompiga risasi wakiwa wamevalia mavazi yao meusi na mahelmet usoni , wakimpiga mwanamke yule anaefanana kwa kila kitu na Edna risasi za

.

mgongoni na mwanamke yule mrembo alievalia mavazi kama ya wakorea(robes) , alidondoka chini huku akiendelea kuliita jina la Roma huku Roma na yeye akijitahidi kutamka neno. “Seven … ntee..n !!” Roma alijikuta akizinduka ghafla , na kujikuta akiwa kwenye masofa huku mke wake akiwa pembeni yake akiwa anamwita kwa wasiwasi huku machozi yakiwa yamejilenga katika mboni za macho yake , aligeuka na kuangalia pembeni na kumuona Bi Wema. “Nini kimetokea mke wangu?”Aliongea Roma huku akionekana ni mwenye kusahau jambo ambalo amelifanya dakika chache nyuma za kutaka kumuua Elvice.

.

“Roma .. haukumbuki kilichotokea?”aliuliza bi Wema huku akionekana ni mwenye wasiwasi sana , ila Roma hakuwa akikumbuka amefanya nini dakika chache nyuma. ,Edna na yeye haikueleweka ni nini kilichompata ghafla kwani alionekana kutoa machozi mfululizo huku akimwangalia Roma pasipo kusema neno , aliishia kunyanyuka mwanadada huyu na kukimbilia chumbani kwake , akimuacha Roma katika hali ya mshangao.

.

“Ndio nakumbuka kulikuwa na mwanaume hapa akipiga stori na Edna na nikamtahadharisha kwa kumwambia aache kuongea maswala ya vita , lakini hakuacha na sikumbuki kilichotokea baada ya hapo”Aliongea Roma huku akimwangalia Bi Wema. “Usijiumize sana kichwa Roma nenda ndani kapumzike”Aliongea Bi wema na kumuacha Roma aende chumbani kwake akapumzike.

.

Roma baada ya kuingia chumbani kwake alionekana kuwa mwenye wasiwasi sana .. kwa tukio alilolifanya muda mchache uliopita.

.

“Inawezekana ugongwa wangu unanirudia”Aliongea huku akisogelea begi lake alilitoka nalo Mbagala Rangi tatu baada ya kuhamia hapo na kuanza kutoa nguo kwa pupa na alionekana ni mwenye kutafuta kitu Fulani kwenye begi hilo na alikipata baada ya dakika chache za kuchanguza. Kilikuwa ni kichupa kidogo mfano wa babycare , lakini kilichokuwa na nembo ya fuvu na X katikati , Roma baada ya kupata Kichupa hiki alionekana ni mwenye kuvuta pumzi ya ahueni. “Angalau hizi dawa zipo nadhani zinaweza kunisadia kwa muda , tatizo hili likiwa kubwa ni hatari kwa binadamu waliopo karibu yangu”Aliongea Roma huku akifungua kikopo hiko na kutoa vidonge vyeusi tii kama mkaa na kuviweka kiganjani mwake.

.

“Lakini nilifanikiwa vipi kurudi kwenye hali yangu ya kawaida gafla sana?”Alijiuliza swali hilo pasipo kujua ni vipi aliweza kurudi kwenye hali yake ya kawaida ghafla , alikuwa hajui kama Edna alimkumbatia kwa nyuma na kumsihi aache ndio wakati alipoacha

.

kweli na macho yake kurudi katika hali ya kawaida na kuzimia. Roma baada ya kufikiria kwa muda , alisogelea tarakishi iliokuwa hapo ndani na kisha aliunganisha na internet

.

baada ya kumaliza alifungua VPN na akaandika maneno flani hivi ya kodi zilizokuwa na mchanganyiko wa XQ na sifuri na nukta nyingi nyingi halafu akabonyeza ‘Enter’ na hapo hapo ikaonekana picha ya Tai mkubwa mwenye rangi nyeusi na nyeupe , ni kama vile unavyofungua Facebook ile picha ya F Inayoonekana ndio kilichoonekana kwenye tarakishi hii. Baada ya picha ile kutokea , ilikuja sehemu ya kujaza jina , na Roma aliandika neno PLUTO na kisha akaweka password yake yenye herufi Zaidi ya ishirini ambazo hazikuwa kwenye mfumo wa mpangiloio yaani kulikuwa na

.

‘Cvbnmejdikeydndyodds’Il ikuwa ni nywira ya aina hio ambayo hata kama unawezo wa kukariri vipi usingeweza kuikariri hio nywira , baada ya kuandika alibonyeza kitufe cha ‘Enter’ na hapo hapo yule mwewe kwa mfumo wa 'animation' alipeperuka na ikatokea video iliokuwa ikimuonesha mwanaume mmoja mwenye ndevu nyingi kama za wataliban lakini mzungu.

.

“Rìgh Pluto Tha còrr air sia mìosan bhon a rinn sinn conaltradh mu dheireadh” “Mfalme Pluto ni Zaidi ya miaka sita sasa tokea tulipowasiliana”. Aliongea yule mzee alieonekana kwenye tarakishi hio akiwa na midevu mingi ya kutisha. “Ndio Sauron , habari za hapo makao makuu ya The Eagles?”Alijibu Roma kwa lufha hio hio “Hapa ni kwema Pluto , hakuna mabadiliko makubwa tokea ulivyotuacha na kurudi kwenye nchi yako kuitafuta familia yako” “Ni vyema kusikia hivyo Sauron , nimefanya mawasiliano na wewe siku ya leo kwakuwa nahitaji msaada kutoka kwako”

.

“Mfalme Pluto hauna haja ya kuomba msaada kutoka kwangu , toa amri nifanye kile unachotaka ,The Eagles ni mtandao wako wa kijasusi uliouanzisha na pesa zako , kwanini uombe msaada kutoka kwangu mimi ni mtumishi wako”Aliongea mwanaume mwenye ndevu ambaye tunamjua kwa jina la Sauron na Roma aliona ni

.

kweli hapaswi kuomba Zaidi ya kutoa oda , alijikuta akitabasamu na kuona kuishi kwa miezi sita ndani ya Taifa la Tanzania kumembadilisha kwani aliwajua wabongo hata kama jambo ni haki yao ya msingi walikuwa wakiomba tofauti na Wakenya na mataifa mengine ambao walikuwa wakihirai sio kuomba.. “Kuna mambo makuu mawili nataka uyafanyie kazi Sauron , jambo la kwanza nataka uangalie The Zeros kuna jambo gani la siri lineandelea”

.

“Mfalme wangu Pluto samahani kama nitakuwa nimevuka mpaka ila naomba ni kuulize kama The Zeros wamefika Tanzania?” “Ndio Sauron , leo walinifanyia mashambulizi ya kushitukiza na walionekana walikuwa na nia ya kuniua kabisa , jambo ambalo limenishangaza, kwanini waanze kunifatilia baada ya kuwa kimya miaka yote hio wakati nilitoka kwenye kundi lao kiamani kabisa na kuunda kundi langu”Aliongea Roma na kumfanya mwanaume aliekuwa akionekana kwenye Tarakishi hio ashangae.

.

’Nitafanya hivyo Mheshimiwa Pluto , nitatuma afisa vipenyo wetu wenye uwezo wa hali ya juu kufatilia nini kinaendelea ndani ya The Zeros , naomba uniambie ni jambo lipi lingine napaswa kufanya” “Nahitaji Mercenary(Masenari) wasiozidi kumi uwatume Tanzania, wakiwa katika mgawanyo sawia wa kimajukumu”Aliongea Roma kwa kilugha na kama ungemsikia ungeshangaa na ukajiuliza huyu jamaa ni nani , kwani aliongea kama anavyoongea Kiswahili. “Hakuna shida The Great Pluto , unataka waje na siraha za aina gani , vifaruu, ndege za kivita au meli?”Roma alijikuta akicheka na kuona Sauron utani wake haujaisha.

.

“Nataka waingie nchini kama watalii wakiwa na silaha za ukimya(silent Weapons) ili wasije wakashikwa kwenye rada za wanausalama wa taifa la Tanzania”

.

“Sawa mfalme Pluto nitazingania hilo na nitafanya arrangement mapema na nitakupa ripoti kesho”. “Nitakutafuta Mimi Sauroni muda wa mchana” “Sawa Mtukufu mfalme Pluto nitahakikisha maombi yako yanafanyika na kujibiwa kwa wakati , naamini huko nchini Tanzania ni usiku , nikutakie usiku kwema” “Na wewe nikutakie asubuhi njema Sauron , wasalimie Watoto wako na mkeo mary”Baada ya maongezi hayo Roma a.k.a Pluto a.k.a Hades alikata simu na kisha kurudi kitandani kukaa chini.

.

“Sina jinsi The Zeros ni ‘Assasination group’ ambalo kama wakiamua jambo lao la kimauji lazima lifanikiwe , mimi ni uzao wao na nimeishi ndani ya uhatari wao na nisipochukua tahadhari mapema Edna anaweza akaingia matatizoni kwa sababu yangu”Aliwaza Roma huku akijiandaa kuingia bafuni kuoga maana mwili wake ulikuwa na maji ya chumvi ya baharini.

.

Upande wa Edna alionekana ni mwenye mawazo sana , kwanza kabisa alikuwa akijiuliza kwanini moyo ulimuuma sana mara baada ya Roma kubadilika na kuwa kama kiumbe ambacho hakina ubinadamu ndani yake , alijiuliza kwanini moyo wake ulikuwa ukimuuma sana mara baada ya Roma kudondoka chini , lakini pia alijiuliza kwanini alivyomkubatia Roma ghafla tu Roma macho

.

yake yalibadilika na kurudi kawaida, lakini pia alijiuliza kwanini alijihisi kitu cha ajabu katika mwili wake baada ya kumkubatia Roma hayo ndio maswali aliokuwa akijiuliza mwanadada huyu nakukosa majibu. NAAAAAM Huu ndio mwisho wa SEASON ONE UKIITAJI KUENDELEA NA SEASON 2 GUSA HAPO CHINI SUBIRI IFUNGUKE

.

ENDELEA KUSOMA ```

Post a Comment

TOA MAONI YAKO HAPA

Mpya zaidi Nzee zaidi

Ads related

Smartwatchs